Involvement

TABIA NCHI

{Picha kwa hisani ya As You Know}

                                               

Na: Gertrude Prosper

{getrude2003@gmail.com}

Tabianchi ni hali ya mabadiliko ya mazingira ya hali ya hewa ikiwemo joto, mvua na pepo. Mabadiliko ya tabianchi yanapojitokeza kunaweza kutokea ongezeko la mawimbi ya joto, mizozo ya kimataifa, mafuriko na ukame unaoathiri viumbe hai.

Kwa asilimia kubwa, mabadiliko haya yanachangiwa na shughuli za binadamu ikiwemo uchomaji wa makaa na mafuta katika viwanda, vituo vya umeme na kwenye magari.

Ongezeko la joto linaweza kuleta athari kama vile; viwango vya maji baharini kupanda, bahari kuchemka na kuwa na tindikali zaidi, barafu vya vilele vya milima kuyeyuka na kusababisha mafuriko, kubadilika kwa mikondo ya bahari, ukosefu wa mvua itakayosababisha njaa na uhaba wa maji, ongezeko la halijoto, upepo, tufani na kuenea kwa magonjwa. Zaidi ya hayo, madhara haya yanaweza kusababisha vifo vya watu na viumbe hai kama mimea na wanyama na kuvifanya kutoweka.

Janga hili la ongezeko la joto linaweza kuepukika ikiwa watu watachukua hatua ya kupanda miti, kupunguza kiwango cha utoaji wa hewa chafu ya kaboni, kukabiliana na matatizo ya taka yanayojikusanya kwenye mito na kupunguza uzalishaji wa gesi chafuzi.

Kando na hayo, watu wanaweza pia kujenga nyumba zinazoweza kumiliki mabadiliko ya tabianchi ili kuwa salama. Njia hizi ikiwemo kujenga kwa kuzingatia ukame, viwango vya joto, mafuriko, baridi, vimbunga na upepo mkali.

Tunatakiwa kuhamisha uwekezaji wetu kutoka kwenye uchumi mchafu kuenda kwenye uchumi msafi unaotumia teknolojia inayowafikia watu wote katika nchi zote.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top