Involvement

ANGELLA OKUTOYI ASHINDA MASHINDANO YA WIMBLEDON

(Picha kwa hisani ya The Standard)

Na Gertrude Prosper

 

Mchezaji wa tenisi, Angella Okutoyi mwenye umri wa miaka kumi na minane aibuka kuwa mwanamke wa kwanza kutoka Kenya kushinda mashindano ya Wimbledon. Katika mashindano hayo ya fainali, Angella alikuwa akishirikiana na Mholanzi Rose Marie Nijkamp katika timu ya wanawake Julai 9, 2022.

Baada ya kushindwa katika seti ya kwanza ya 3-6 Okutoyi pamoja na mchezaji mwenzake waliamua kujikakamua na kushinda seti ya pili. Wapinzani hao, Kayla Cross na Victoria Mboko walishindwa (11-9) dhidi ya Nijikamp na Okutoyi (3-6, 6-4).

Angella amevunja rekodi na kuwa Mkenya wa kwanza kufika katika fainali , akishirikiana na mwenzake Rose Marie, baada ya kuwashinda wapinzani wao Nikola Daubenova kutoka Serbia na Circa Bagaric kutoka Kroeshia (6-3 6-4) katika nusu finali.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top