Involvement

WAZIRI MKUU WA ZAMANI WA JAPAN, SHIZO ABE AFARIKI DUNIA.

(Picha kwa hisani ya OneIndiaNews)

Na Gertrude Prosper

 

Waziri Mkuu wa zamani wa Japan, Shinzo Abe amefariki dunia baada ya kupigwa risasi akiwa katika kampeni za chama chake cha Liberal Democratic Party (LDP) kwenye uchaguzi wa wabunge katika mji wa Nara Magharibi mwa nchi hiyo.

Abe amefariki dunia hospitalini baada ya kulazwa akiwa mahututi kufatiwa kupigwa risasi katika mashambulizi hayo. Katibu Mkuu wa nchi ya Japan, Hirokazu Matsuno pamoja na Waziri Mkuu Fumio Kishida wamesema hali ya Abe ilikuwa mbaya baada ya kupata shambulio la moyo.

Mshambuliaji huyo ameshakamatwa na maafisa wa usalama na walinzi wa Abe muda mfupi baada ya shambulio hilo.

Shinzo Abe ni kiongozi wa zamani wa Japan kutumikia nchi hio kwa muda mrefu zaidi kuliko mawaziri wakuu wengine wote nchini humo. Abe alizaliwa Septemba 21 1954 jijini Tokyo na alianza harakati za kisiasa 1993 alipoteuliwa kuwa mwakilishi wa baraza la juu la bunge kisha akateuliwa kuwa katibu mkuu wa baraza la mawaziri Septemba 2005 kabla ya kuja kuchukua nafasi ya urais wa chama chake cha Liberal Democratic Party (LDP) mwaka 2006. Abe anatoka kwenye familia ya kisiasa ambapo babu yake alikua Waziri wa nchi hio kwanzia mwaka 1957 hadi mwaka 1960 na baba yake alikua katibu mkuu wa baraza la mawaziri la nchi hiyo, cheo ambacho kinaonekana ni cha pili kwa ukubwa zaidi nchi humo. Abe alikua Waziri mkuu wa Japan akiwa na miaka hamsini na miwili mwaka 2006, kiongozi wa kwanza kijana kuchukua nafasi hiyo. Muhula wake wa kwanza madakarakani uliubikwa na majanga kutokana na matatizo yake ya kiafya na kumfanya ajiuzulu. Alirejea tena serekalini na kutumikia wadhifa wa Waziri Mkuu katika nchi ya Japan kutoka mwezi Disemba mwaka 2012 hadi mwezi Septemba mwaka 2020.

Abe atakumbukwa kwa sera yake ya kiuchumi akijaribu kufufua uchumi wa Japan uliokua umedorora. Atakumbukwa pia kwa kuongeza bajeti ya ulinzi na kubadili sera ya kijeshi ya Japan iliyodumu kwa miaka sabini. Alipambana pia kuboresha mahusiano yake na China.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top