Involvement

Sherehe ya Eid-ul-Adha 2022

(Picha kwa hisani ya Hindustan Times)

Na Getrude Prosper

Mwaka huu wa 2022, nchi tofauti tofauti duniani zimesheherekea sikukuu ya Idd kwenye tarehe tofauti. Baadhi ya nchi zimesherehekea siku ya Jumamosi Julai 9 2022 na zingine zimesherehekea siku ya Jumapili Julai 10 2022. Zaidi ya hayo, Waziri wa Usalama wa ndani, Fred Matiang’i ametangaza kuwa Jumatatu, Julai 11 2022 kuwa siku ya mapumziko ya kuadhimisha sikukuu ya Idd-ul-Adha nchini Kenya.

Idd-ul-Adha ni siku ya kuchinja na huadhimishwa siku ya 10 ya Mwezi wa Dhul-hijjah, mwezi ambao waislamu huenda kuhiji Makka, Saudi Arabia. Sherehe za mwaka huu nchini Kenya zimekua tofauti kidogo kutokana na hali ya uchumi iliyofanya gharama ya maisha kua juu. Baadhi ya wafanyabishara wanadai kua msimu huu wamepata hasara kubwa kwasababu ya kupungua kwa wateja. Kabla ya mabadiliko ya hali ya uchumi, siku za sherehe hua ni siku za wafanyabiashara kuuza zaidi kuliko siku zingine kutokana na misururu ya watu wanokuja sokoni kununua bidhaa mbambali ikiwemo nguo na vyakula.

Mwaka huu hamna dalili zozote zile za sherehe kwenye baadhi ya maeneo kama awali kutokana na gharama ya maisha kupanda. Vitu vimepanda bei wanunuaji wamepungua.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top