Involvement

UONGOZI UPYA KATIKA KLABU YA DAYSTAR COMPASSION AND CARE CENTER

Na Gladys Sheila
gladyshila52@gmail.com

Picha kwa hisani ya: Joseph Gichari

Josephndungo55@gmail.com

Klabu ya Daystar Compassion and Care Center (DCCC) almarufu DC3 iliyoko katika chuo kikuu cha Daystar ilisherehekea uongozi upya. DC3, ni klabu ambayo imekuwepo tangu mwaka wa (2013) huku lengo lake kuu likiwa kufahamisha wanadaystar kuhusu maswala ya afya, kuwasaidia kisaikolojia wanafunzi, wahadhiri, wafanyakazi na jamii ya Daystar kwa ujumla. Klabu hii imekuwa chini ya uongozi wa Bi.Susan Botto ambaye ndiye mratibu wake.

Siku hii ya ndovu kumla mwanawe, iliyoadhimishwa katika chapeli iliwaorodhesha viongozi wake wa mwaka wa 2019-2020 huku waliowatangulia wakiwakabidhi faili za utendakazi wao. Siku hiyo ya aina yake ilianzishwa kwa tenzi za kumsifu na kumuabudu Mungu, hafla iliyoongozwa na kwaya ya Imela katika chuo kikuu cha Daystar. Hali kadhalika, wanafunzi, wahadhiri na wafanyakazi chuoni Daystar walipokea pipi huku ikiwa kiishara kuwa wasiokwenye ndoa wajihifadhi mpaka wakati wa kufunga ndoa.

Kilele cha hafla hii ni ufahamu dhabiti wa klabu hicho na wanajopo ambao walikuwa Bi. Emmah Nguli na Bwana Allan Ball ambao ni washauri wa maswala ya saikolojia.

Matayarisho ya siku hii isitoshe hung’oa habta wiki ikianza huku mada kuu ikiwa kuwahamasisha wanadaystar kufahamu afya zao. DC3 hukakisha kuna vitengo mbalimbali ambavyo vyaweza kuwasaidia kutambua hali zao za kiafya ikiwa upimaji wa ongoezeko au upungufu wa sukari mwilini, uchunguzi wa saratani, kuangaliwa meno na upimaji wa ukimwi. Ukabidhishaji wa nyara kutoka kwa naibu wa msimamizi mkuu wa wanafunzi Bi. Irene Kimani.

Waliotuzwa walikuwa:
1. David Obong’o- Rais
2. Gladys Sheila- Naibu wa Rais
3. Wilbert Kiprop- Katibu
4. Kevin Korir- Mweka Hazina
5. Maureen Minus- Mkurungezi wa Halfa
6. Chris Waweru- Msaidizi wa Vikundi vya Msaada

Erick Spira, rais anayeshika timu hiyo mpya mkono, aliwapongeza waliomtangulia na kuwahamasisha wanafunzi kuridhika kwa kasoro wanazojua wanazo kwani zina manufaa maishani. Kwa kuwa chanzo cha jambo ni mwisho wa kingine, timu hiyo ilijumuika na kukata keki ya kusherehekea uongozi upya na uliopita katika ofisi zao za DCCC.

Kweli sote kama wanafunzi, wahadhiri na wafanyakazi twawatakia viongozi hao kila la heri wanapoongoza wanadaystar.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top