Involvement

SHUJAA WETU

Na: Wangu Kanuri

kanuriwangu@gmail.com

Melina Gold, mwanzilishi wa begi za Melina Gold.

TUELEZE kuhusu ushoni wako wa mikoba [UTANGULIZI]

Mikoba ya Melina Gold, ninashona kwa kutumia ngozi. Utengenezaji wa mikoba hii ilianza mwaka wa 2019 Februari huku lengo langu likiwa kuutuza usanii na upekee wa vitu vya Kenya. Ushonaji wa mikoba hii hutumia ngozi na mshoni wangu ndiye hukarabati usanii kadha wa kadha.

TUELEZE kwa ufupi kukuhusu

Jina langu ni Melina Gold na mimi ni mwanafunzi wa mwaka wa nne katika chuo kikuu cha Daystar. Ninafanya shahada yangu katika mawasiliano kitengo cha uhusiano wa umma na nyongeza ya masomo katika saikolojia.

NINI kilikuchochea kuupenda kushona mikoba?

Ushoni wangu unanuia kuhamasisha wakenya kupenda na kuonea fahari mikoba ya Kenya kwa hivyo nikachukua jukumu hili kuzitengeneza mikoba ambayo itafifisha uduni wa bidhaa za Kenya. Hali kadhalika, nilitaka kuwazindua wanabiashara kujikita katika utengenezaji wa mikoba ili kuongeza mikoba yenye asili ya Kenya kwenye soko.

NI changamoto zipi unakumbana nazo katika ushoni huu?

Kutompata mshoni ambaye amebobea katika ushoni, kutowajibika kwa washoni ambao aghalabu hutumia ngozi hii kushona bidhaa nyingine zao bali si mikoba yangu, kutopata ngozi hii ya kutumia katika ushoni na kutopata watu ambao wanamaono sawa na yangu katika utengenezaji huu wa mikoba.

MIKOBA yako ni ya aina gani?

Melina Gold ni mikoba ambayo hutumia ngozi.

UNAWASHAURI vipi wanabiashara chipukizi?

Wasitegemee wanadamu kwani aliyemfunza chui kumla binadamu ni mtu. Pili waangaze maono yao kwa kina na wasiangeme. Mwisho wawe wenye bidii katika kuhakikisha biashara zao zimekua.

Wasiliana na Melina Gold Kupitia:

+254706602386

@melinagoldbagline on instagram

1 thought on “SHUJAA WETU”

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top