Involvement

TATANISHI LA MAFURIKO MJINI MOMBASA

 

Na Ashley Mbashu

 

Kulingana na taarifa za hali ya anga, sehemu tajika za kaunti ya Mombasa zimeshuhudia mvua ya  mno.

 

Mafuriko yanaendelea kuzua misukosuko mjini Mombasa. Baadhi ya mikoa iliyoathirika kupita kiasi ni eneo la Bamburi, Old Town na kwingineko.

Takwimu za serikali zinaarifu kuwa kaunti 33 zimeathirika kutokana na mvua kubwa

 

Idadi ya vifo yasemekana kufika watu sitini na mmoja, wanane hawajulikani waliko,waliojeruhiwa 235  kutokana na mvua hiyo. Nyumba zilizoathirika ni 80518, biashara  143, vituo vya afya 25, vituo vya mifugo 11610,shule 10. Miongoni mwa walioripotiwa kupotea ni maafisa wawili wa halmashauri utozaji ushuru KRA, gari lao kusombwa na maji eneo la Ramisi katika Lungalunga walipokuwa wakisafiri kuelekea Mombasa.

 

Serikali za kaunti zashauri walio maeneo hatari kuhamia maeneo salama. Hamasisho latolewa wenye magari kuwa waangalifu zaidi.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top