Involvement

Penzi Halijaribiwi, Utanaswa Unasike.

(Picha kwa hisani ya The Economic Times)

Na Abdul Shaban

 

Mapenzi ya siku hizi, ni ya nipe ndo nikupe,

Tena ya tele mapozi, kadhalika na mapepe,

Sipo jali tawa chizi, ujipake na matope,

Penzi halijaribiwi, utanaswa unasike.

 

 

Penzi halina mjuzi,  nina kwambia peupe,

panga yako mamuzi, mabaya uje utupe,

ya sikutoke machozi, yakalovya zako hope,

Penzi halijaribiwi, utanaswa unasike.

 

 

Mapenzi toka awali, yaliwashinda wa kale,

Usijione mkali, utarudi na tandale,

Samsoni nguvu kali, alinaswa palepale,

Penzi halijaribiwi, utanaswa unasike.

 

 

Ukijifanya bahili, kutosikia wavyele,

Utashikika pahali, upige zako kelele,

Kusifiwa ni muhali, huwezi kusonga mbele,

Penzi halijaribiwi, utanaswa unasike.

 

 

Kujipiga na kifua, eti wewe umakini,

Utakuja kujutia, ushindwe na kibaini,

Utalia na dunia, uhame nako nyumbani,

Penzi halijaribiwi, utanaswa unasike.

 

 

Mwisho nikimalizia, kwa huu wangu waraka,

Polepole kuanzia, sikuwa nayo haraka,

Nadhani mumesikia, madada na kina kaka,

Penzi halijaribiwi, utanaswa unasike.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top