Involvement

Matokeo ya siku ya Jumatano

[Picha kwa hisani ya AFC]

Na Dennis Mungai 

Mabingwa mara kumi na tatu Real Madrid walipata ushindi wa bao moja kwa bila dhidi ya Union Berlin. Jude Bellingham alifunga bao la pekee mechi ilipokaribia kukamilika na kuipa Los Blancos alama tatu. Arsenal walianza msimu wao kwa kishindo huku wakigaragaza PSV 4-0. Mabao ya Arsenal yakifungwa na Saka, Martin Odegaard, Jesus na Trossard. Inter Milan walitoka sare ya bao moja na Real Sociedad nayo mechi ya Sevilla na Lens kukamilika sawia.

Napoli walishinda Braga mabao mawili kwa moja, Galatasaray walitoka sare ya mabao mawili dhidi ya Copenhagen na Salzburg walishinda Benfica 2-0. Mechi ya siku ilikua kati ya Bayern Munich na Manchester United. Vijana wa Erik Ten Hag walianza kwa kishindo lakini Bayern walifunga bao la kwanza kupitia Leroy Sane.

Katika dakika za mwisho Matheus Tel na Casemiro walifungia timu zao lakini mechi ilikamilika Bayern wakipata ushindi wa 4-3. Harry Kane na Serge Gnabry pia walifungia Bavarians. Raundi ya kwanza ya michuano ilikamilika jana na mkondo za mechi za Europa zinatarajiwa kuanza siku ya Alhamisi.

 

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top