Involvement

MAKAMU CHANSELA WA CHUO KIKUU CHA DAYSTAR ATEULIWA KAMA MWAKILISHI WA KITAIFA WA BODI YA CHAMA CHA ELIMU YA MAREKEBISHO, MAREKANI.

[Picha kwa hisani ya Prof. Laban Ayiro Facebook]

 

Na Ashley Mbashu

 

Makamu wa chansela, Profesa Laban Ayiro, ateuliwa kuwa mwakilishi wa bodi ya chama cha Elimu ya Marekebisho,  Marekani.

Chama hiki kinahusu wataalamu wanaofanya kazi kwenye vitengo vya watu wazima na watoto kote nchini. Wao hutoa mafunzo muhimu na mitandao yenye manufaa ili kuwawezesha kuwasilisha maelekezo yenye ufanisi na yenye kuleta mabadiliko kwa wanafunzi wao.

Shirika hili la kimataifa kiliundwa mnamo mwaka wa elfu moja mia kenda na thelathini. Shirika hili limeweza kuwahudumia watoa nidhamu na mashirika ya elimu ya mabadiliko kote duniani kwa miaka mingi.  Limeweza kutimiza haya yote kupitia uongozi, mwelekeo na huduma wanazotoza. Shirika hili limeibuka la kipekee kwenye utetezi wa kitaalam nchini Marekani.

 

Kama mwakilishi wa kimataifa wa chama husika, Profesa Laban ana jukumu la kuhakikisha uhusiano mwema kati ya shirika husika na mashirika mengine ya kimataifa,  na taasisi zinazohusika na elimu ya marekebisho na nyanja zisizo za Marekani. Pia, atatakiwa kurahisisha mawasiliano kati ya shirika la kimataifa na washirika wao wa kimataifa.

 

Profesa Ayiro pia atahitajika kuwakilisha muungano kwenye mikutano ya kimataifa na mingine ambapo pia atatakiwa kushiriki maarifa na kuzungumza kwa niaba ya wanachama wa shirika hilo.

 

Kuteuliwa huku kwa Profesa Ayiro kwenye nafasi hii kunaonyesha anavyojizatiti kwenye kazi zake na pia uongozi. Ni heshima na fursa kuu kwetu, wanafunzi wa chuo kikuu cha Daystar, kwani tutaweza kujifunza na pia kufuata nyayo zake. Uteuzi huu ni ushahidi wa mafanikio yanayoweza kufanikishwa kupitia bidii za mchwa, kujitolea na cha muhimu, dua.

 

Sisi kama wanachama wa gazeti la Involvement, tunampa mkono wa pongezi, Makamu chansela, Profesa Laban Ayiro.

 

Kongole!

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top