Involvement

   AFYA YA AKILI

(Photo courtesy of uCheck Blog)

Na: Gertrude Prosper

getrude2003@gmail.com 

Afya ya kiakili ni hali ya kuwa sawa kiakili, kisaikolojia na kuwa na mawazo chanya. Afya ya kiakili ni muhimu kwa sababu inahusiana na jinsi akili ya mtu inavyofanya kazi.

Miaka inavyozidi kuenda, afya ya kiakili inaharibiwa na hivyo kusababisha watu kupata matatizo ya kiakili. Matatizo haya ya kiakili hayachagui jinsia, aina ya kazi mtu anayofanya wala umri, mtu yeyote anaweza kupata, sanasana vijana ndio wanaonekana kuathirka kwa asilimia kubwa. Watu wengi wamezoea kupuuzia kuhusu afya ya akili zao na hii imewafanya kugundua kua wanamatatizo ya kiafya baadae wakati wameshachelewa.

Mwelekeo wa matatizo ya afya ya kiakili duniani unazidi kutia shaka kutokana na idadi ya watu inavyozidi kuongezeka. Wataalamu wa afya ya kiakili wanatakiwa waongeze bidii ili kutoa matibabu na huduma dhidi ya vyanzo vya matatizo ya akili. Sio waatalamu tu, hata ndugu, jamaa na marafiki wanaweza kuwa msaada mkubwa kwa watu hawa.

Vyanzo au vichochezi vya matatizo ya kiakili ikiwemo ukatili wa kingono/ kijinsia, uonevu, unanyasaji, unyanyapaa, ubaguzi, ugumu wa maisha na ukiukaji wa haki za binadamu. Vyote hivi vinaweza kumsababishia mtu kupata matatizo ya afya ya kiakili. Kando na hayo, huzuni, kusononeka, hofu, woga na hasira ya kila wakati vanaweza kua ni vyanzo vya matatizo ya akili.

Vyanzo wengine ni migogoro katika familia ikiwemo wazazi au walezi kugombana mbele ya watoto, kuwapiga watoto wao au kutumia lugha isiyofaa kwa watoto. Hii inaleta matatizo ya kisaikolojia kwa watoto. Wazazi au walezi wanatakiwa kua mifano bora kwa watoto kwasababu hawa ndio vijana watakaokuja kuteseka kiakili baadae. Wazazi wanatakiwa wahakikishe kuwa wao ndio mstari wa mbele kuwalinda na kuwajengea watoto mienendo na maadili inayofaa katika maisha. Vijana ndio taifa la kesho.

Athari za kutoshughulikia matatizo ya afya ya kiakili husababisha mambo makubwa kama vile kuleta misongo ya mawazo, kiwewe, kuwalazimu watu kujiua na matumizi ya pombe na mihadarati.

Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwepo kwa ripoti nyingi za mauaji kutokana matatizo ya kiakili, na bara la Afrika likiwa linaongoza kuliko mabara mengine duniani. Takriban zaidi ya watu 10 kati ya 100,000 hufa barani Afrika, ambayo ni zaidi ya wastani wa kimataifa. WHO imesema kuwa Afrika ina uhaba wa matibabu na huduma wa magonjwa ya afya ya kiakili, hii ni kutokana na imani potofu zinazowafanya watu kupuuzia magonjwa haya. Watu hawa wanapokosa msaada wanalazimika kujiua au kufanya matendo ya kujiumiza.

Mtu anapoishi kwa huzuni mwingi, kukosa usingizi, kua na mshtuko, mawazo mabaya, upweke, dhiki, wasiwasi au kusikitika kushusu maisha, ni vizuri kutafuta msaada mapema kabla ya kufanya mambo ya kujiumiza.

Matibabu ya kiakili na huduma ni pamoja na kuzungumza au kuwasiliana na watu unaowaamini ikiwemo marafiki, familia, wahudumu wa afya, na wakijamii. Mawasiliano kwa kawaida ni kwa ajjili ya kupashana au kubadilishana habari, hisia, maoni au mawazo kwa kutumia maneno, maandishi au ishara.  Watu wengi hushindwa kuwasilisha hisia zao kwa muda unaofaa na hii huwasababishia madhara mengi ikiwemo afya ya kiakili. Wengi wao huona ni vigumu kujielezea kwa wengine kutokana na aibu au kutotaka kuonekana wadhaifu. Utayari wa kuzungumza ili kutafuta suluhisho ni hatua muhimu sana, kwasababu inaweza kumsaidia mtu kuepuka kujiua au kupata misongo ya mawazo.

Ni sawa kutokua sawa, hauko pekee yako. Tafuta msaada mapema.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top