Involvement

SIKUKUU YA MOI YAREJESHWA TENA

Picha kwa hisani ya: businesstoday.co.ke

Na Gladys Sheila,
gladyshila52@gmail.com

Katibu wa baraza la mawaziri katika wizara ya mambo ya ndani na uratibu wa serikali ya kitaifa Daktari Fred Matiang’i alitoa taarifa siku ya Jumanne na kuidhinisha sikukuu ya Moi kama sikukuu ya kitaifa.

Hii ni baada ya uamuzi wa mahakama. Mnamo mwaka wa 2010, sikukuu ya Moi iliondolewa katika orodha ya sikukuu za kimataifa wakati katiba mpya ilizinduliwa rasmi. Mwezi wa Novemba mwaka wa 2017, jaji wa mahakama kuu alipinga uamuzi huo kwa kusema kuwa ni jambo ambalo linakiuka sheria. Mojawapo ya sababu ilikuwa kuwa sikukuu ya Moi haikuwa ya kuadhimisha wananchi au ufanisi wa nchi, bali mtu mmoja.

“Kulingana na sheria kuhusu Sikukuu (Sura ya 110, Sheria za Kenya) na uamuzi wa mahakama katika Kesi ya Kikatiba Nambari 292 ya 2017, ninatangaza kuwa Oktoba 10, 2019, itakuwa sikukuu ya kitaifa,” Waziri Fred Matiang’i akasema.

Hata hivyo, Wakenya wengi walikuwa na njia anuwai za kusherehekea siku hiyo. Wengine waliendeleza biashara zao kama kawaida, wengine wakisafiri kukutana na jamaa na familia zao na wengine wakapumzika kutoka kazini.

Liliofanya sikukuu hii iwe ya kipekee ni kuwa wakenya wengi walitumia muda huu kuwatembelea na kuwapa msaada watoto katika nyumba za mayatima, wajane, wazee waliotengwa na familia zao, walemavu na wengineo kama ishara ya upendo.

Hali kadhalika, wakenya wengine walikuwa na msimamo tofauti kuhusu maadhinisho ya sikukuu hiyo huku wakifananisha kipindi cha uongozi wa Mheshimiwa Moi kama dikteta.

Picha kwa hisani ya: Nairobinews.nation.co.ke

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top