Involvement

Prof.Laban Ayiro azungumzia Elimu ya Utatuzi chuoni Daystar

Na; Righa Sedellar

Profesa Laban Ayiro – Naibu Chansela.

Hivi leo katika makala ya Dau La Elimu na Frank Otieno kwenye runinga ya KTN, Naibu Chansela wa chuo kikuu cha Daystar,Profesa  Laban Ayiro pamwe na Mhadhiri wa chuo kikuu cha Moi,Profesa Violet  Naanyu  na Profesa Lukoye Atwoli wa chuo kikuu cha Aga Khan walichangia pakubwa katika mjadala wa Elimu Ya Utatuzi Masuala (Problem based learning) na kusisitiza kuwa, mfumo huu wa elimu una faida nyingi sana katika maisha ya mwanafunzi.

Elimu ya utatuzi masuala ni mfumo wa elimu unaolenga kutengeneza binadamu  anayeweza  kutatua matatizo mbalimbali ya kijamii,anayeweza kujimudu maishani na mwenye maadlili yanayoweza kutegemewa nchini na ulimwenguni.

Profesa  Laban Ayiro alisisitiza kuwa chuo kikuu cha Daystar kimeshachukua mkondo huu wa mafunzo na kusema,”Katika chuo cha Daystar  Walimu huwa wanaenda madarasani ,wanawapa wanafunzi maswali na kuwaaacha wajadiliane na kutatua matatizo mbalimbali kisha kusahihisha matokeo yao kwani  nia yetu ni kutoa wanafunzi walio kamili baada ya kumaliza masomo yao katika chuo kikuu cha Dasystar”.

Vilevile,wenza wake Profesa Ayiro walisisitiza kuwa,mfumo huu wa elimu unaweza kuwa wa manufaa zaidi japo walimu  pamwe na serikali yetu ya Kenya itatilia mkazo na kuhakikisha kuwa mfumo huu wa elimu umetiliwa maanani na kila mwalimu kutumia mfumo huu kuwaelimisha wanafunzi vyuoni.

Aidha ,jopo hili la wataalam wa Elimu lilisisitiza kuwa,kuna haja kubwa sana ya walimu kunolewa zaidi na kufunzwa mfumo mpya  wa elimu ili nao pia waweze kuwafunza wanafunzi vyuoni kwani walimu wa sasa walifunzwa mfumo tofauti wa enzi zao. Imekuwa changamoto kubwa sana kwa walimu hawa kuwafunza wanafunzi kutumia huu mfumo mpya wa elimu.Fauka ya hayo,Profesa Violet Naanyu  alisisitiza kuwa elimu huwa ni safari  kwani huwa kuna mwanzo na huwa kuna lengo kuu la mwanafunzi anaposoma na mwalimu anapofunza. Kwa hiyo,Violet alilonga kuwa kuna umuhimu wa walimu kuwa na ushirikiano na wanafunzi ili pamoja waweze kukamilisha ‘safari’ ya  elimu aisee! Kidole kimoja hakivunji chawa .

Kaditama,wataalam hawa walitoa maoni yao na kusema kuwa ,japo tunataka mfumo huu wa elimu kutufaidi ifaavyo, itabidi viongozi wa vyuo wafunzwe mbinu mpya ya uongozi. Viongozi wawe wanaokubali maendeleo na kuhakikisha kuwa maendeleo tofauti yanatekelezwa katika vyuo wanavyosimamia.

Wakufunzi nao  wawe tayari kujadiliana na kukosoana na wanafunzi wasiwe na akili ya kufikiri kuwa ni wao pekee wanaojua yote. Wanafunzi pia walihimizwa kuwa na bidii za mchwa na wawe watu wa kutaka kujua mengi, wafanye utafiti na kutumia utafiti huo kutatua matatizo mbalimbali.

Kwa uhahika,mjadala huu ulikuwa na mafunzo chungu  nzima na ni ombi langu kuwa wewe kama msomaji wangu utaweza kuyatilia maanani yaliyosemwa na wataalam na kuhakikisha kuwa, polepole  na kwa uhakika unakubali mfumo mpya wa elimu kwani mfumo huu una manufaa kadha wa kadha.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top