Involvement

Matokeo na matukio Ligi Kuu Uingereza

 

Na Dennis Mungai

 

Raundi ya kumi na sita za mechi ligi kuu nchini Uingereza ilikamilika jana usiku baada ya mechi baina ya Liverpool na Manchester United. Mechi hiyo ilitoka sare tasa huku vijana wa Erik Ten Hag wakiweka ulinzi uliokua mgumu kupitwa na mashambulizi ya Liverpool. Diogo Dalot wa United alipewa kadi nyekundu katika dakika za mwisho lakini bado vijana wa Klopp hawakupata nafasi ya kufunga bao. Matokeo hayo yanawaacha Liverpool katika nafasi ya pili nayo United kushuka mpaka nafasi ya saba.

Kwingineko, Arsenal walimaliza wikendi katika nafasi ya kwanza katika jedwali baada ya kuipiga Brighton 2-0. Mabao ya Jesus na Havertz yaliipa timu yao alama tatu kabla ya kumenyama na Liverpool siku ya Jumamosi. West Ham waliiduwaza Wolves 3-0 nayo Aston Villa iliendeleza msururu wa matokeo mazuri kwa kuipiku Brentford 2-1.

Siku ya Jumamosi,  Chelsea ilishinda Sheffield United 2-0, huku mchezaji mpya Christopher Nkunku akirudi kikosini ila hakucheza mechi hiyo. Newcastle walizidi nguvu Fulham baada ya kutolewa katika mashindano ya  ligi kuu ya Mabingwa Ulaya, vijana wa Eddie Howe wakipata ushindi wa mabao tatu bila jibu. Everton walipiga Burnley mabao mawili kwa bila nayo Spurs kuilemea Nottingham Forest kwa matokeo sawia siku ya Ijumaa.

Mabingwa watetezi Man City walipoteza alama nyingine baada ya kutoka sare ya mabao mawili dhidi ya Crystal Palace. Grealish na Rico Lewis waliipa City uongozi lakini Mateta na Olise walifunga katika dakika za mwisho kujinyakulia alama moja. City sasa wapo katika nafasi ya nne kabla ya kuenda nchini Saudi Arabia kucheza michuano za FIFA Club World Cup.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top