Involvement

KIVUKIO CHA KIFO

Na: Dorothy Waweru
dorothywaweru161706@daystar.ac.ke

Picha kwa hisani ya: The Star

Ni afueni kwa wakenya wote na haswa familia yake Bi. Mariam Kighenda kwa kutolewa katika hindi la Victoria.

Shughuli hii iliyochukua siku kumi na tatu, imezifanya nyoyo nyingi sasa kupata na utulivu. Aila ya Bi. Mariam sasa inauhuru wa kuzipumzisha mili ya wapenda wao ambao wamesumbuka usiku kucha. Japo bado uchungu upo, tunamwomba Mwenyezi Mungu aweze kuilaza roho zao pahala pema peponi.

Hata hivyo, Shirika la Kenya Ferry limekabiliwa na mashtaka chungu nzima kufuatia ajali iliyotokea katika kivuko cha Likoni. Ajali hiyo ilihusisha kutumbukia kwa gari moja kwenye bahari hindi mnamo Septemba ishirini na tisa mida ya saa kumi na mbili. Gari hilo lilikuwa na abiria wawili, Bi. Mariam Kighenda na mwanawe Amanda Mutheu.

Yasemekana wawili hawa walikuwa wametoka kuzuru shamba katika kaunti ya Kwale na walikuwa wakirejea nyumbani walipopatana na kifo chao.
Matukio yaliyojiri baadaye yanaashiria utepetevu mkuu wa shirika la Kenya Ferry katika kutekeleza majukumu yao ya kuhakikisha usalama wa wasafiri.

Baada ya ajali hiyo kutokea siku ya Jumatatu tarehe thelathini Septemba, Kenya Ferry kupitia mtandao wa kijamii wa twitter ilitangaza kuwa watahakikisha kuna meli nne katika kivukio cha Likoni.

Wakenya kupitia mtandao huo walituma jumbe zilizosheheni kughadhabishwa kwa usemi wa Kenya Ferry kwani la muhimu lilikuwa kuomba msamaha kwa familia ya walioadhirika badala ya kuwaambia wananchi kuwa feri nne zitatutumika kuwasafirisha abiria hapo likoni.

Ni jambo la kukereketa maini kugundua kwamba shirika la feri halina mikakati bomba inayowahakikishia abiria usalama wao hasa wakati kuna tukio kama hilo linalohatarisha maisha yao.

Uchunguzi ambao unaendelea kufanywa umebaini kwamba shirika la feri la humu nchini halina wapiga mbizi ambao wanasafiri katika feri mchana na usiku bali wanawategemea wapiga mbizi katika shirika la Kenya Ports Authority na jeshi la baharini humu nchini.

Uhai wa mama Amanda na mwanawe haungekatizwa ghafla iwapo shirika la Kenya Ferry lingekuwa na wapiga mbizi katika chombo hicho wakati wa mkasa huo. Wapiga mbizi wangelikuwepo wangefanya hima kuwaokoa abiria hawa punde tu gari lao lilipoanza kuzama.

Msemaji wa serikali Col Rtd, Cyrus Oguna alipokuwa akitoa taarifa aliwaambia wanahabari kuwa gari lilichukua chini ya dakika moja unusu kuzama kwa hivyo kulikuwa na muda tosha wa kuwaokoa wasafiri hawa.

Sababu za kucheleweshwa kwa kutolewa kwa miili ya walioaga ni kuwa kuna meli zinazopita baharini kupitia bandari ya Mombasa kufanya biashara ambayo inailetea kaunti ya Mombasa fedha nyingi. Tunaelewa kwamba tukikatiza usafiri wa meli baharini uchumi wa Mombasa utaadhirika pakubwa.

Sababu ya pili ni giza kali ambayo imeshuhudiwa baharini hivyo wapiga mbizi wanatatizika sana. Tatu ni mawimbi makali yanayovuma baharini hivyo shughuli za uokoaji zinagonga mwamba wakati huo hadi mawimbi yatulie. Lakini ile sababu muhimu zaidi ni kuhakikisha kuwa usalama wa wapiga mbizi na wale wote wanaohusika katika shughuli za uokoaji unadumishwa,” haya yalikuwa maoni ya msemaji wa serikali Col Rtd.Cyrus Oguna.

Shirika la Kenya Ferry limeshuhudia visa kama hivi vya ajali bali ni hatua chache sasa zimechukuliwa kuimarisha utendakazi wao. Wasafiri hawana uhakika wa usalama wao kwani janga kama hili linaweza kutokea bila usaidizi wowote. Ni bayana kuwa uwepo wa kuwa tayari kukabiliana na mikasa ya baharini ni jambo linalofaa kutiliwa mkazo.

Feri zote zinafaa kuwa na vyombo vya kuhakikisha usalama wa wasafiri na magari pia. Sheria mpya zinafaa kubuniwa ili kuwe na mpangilio katika feri hizi. Hakuna mtu ambaye anafaa kupoteza maisha yake kupitia kisa cha kuhuzunisha kama hiki.

Picha kwa hisani ya: citizentv.co.ke

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top