Involvement

ENYI VIJANA

(Picha kwa hisani ya Owlcation.com)

Na Abdul Shaban

 

Tulisifu na kulitukuza jina lake siku zote

Kwa maana anatupenda sisi sote

Uwepo wake umedhihirika kote duniani

Siku zote nuru za nguvu zake huonekana hata gizani

Wakati wa furaha na majonzi na dhiki

Yeye ndiye dereva wa maisha yetu

 

Enyi vijana, njooni nyote kwake Jalali

Yeye ndiye mweza wa yote na aliye halali

Tujiepushe na yale yanayomchukiza

Tuwe tayari tuitwapo kusikiza

Yake masharti kuyafuatilia daima

Ili maisha yetu yaweze kusimama hima

 

Enyi vijana, tuwe chombo cha kueneza amani

Ili mioyo ya wazee na kote duniani iwe na furaha isiyo na kifani

Tujiepushe na yale yanayoeneza chuki

Bali tulitengeneza chakula cha ujirani wema kama asali kwa nyuki

Tupige magoti tusali kwa Mola tukiomba dua

Kuwa kila siku tuweze kuvutia kama ua

 

Enyi vijana, yakini tukumbuke tulikotoka

Tubadilishe yetu mienendo ili tupate kuokoka

Tusiwe na mioyo mizito ilijaa takataka

Bali tuombe msamaha kwake Mola mkono wake wa kulia tutakaa

Tuweze kusimama imara katika imani yetu

Tukijua ya kwamba mola hujibu maombi yetu

Na yule amwaminiye hawezi kumwacha ateseke kamwe.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top