Involvement

Sikitiko la moyo

Na Mariita Joshua 

Langu sikitiko ni haja ya moyo,

Moyo wenye kuvunjika na kuvunda,

Makovu yangalipo kama alama ya utambulisho.

Nisijafa ili nililiwe ila vikao naviona jinamizini,

Furaha imenikoma ili wimbi la kiza litawale,

Nani wakunipa mapendo ili mtima udunde?

Mbona raha inikauke wakati chemichemi inabubujika?

Nguvu sinazo, ni lelemama jina langu,

Hawahitaji kwenda vichekeshoni,

Mwenyewe ningalipo kitimbwi,

Pembeni nimevikwa kirauni, mashaka mie!

Kama matambara nimeraruka,

Afadhali nipige deki matapishi yalozagaa sakafuni,

Nikanyagwe na wenyeji kwa wageni,

Nitumbukizwe majini niloe nifinyangwe.

Wakila vitamu nilambishwe munyu,

Niwe na ndia ndefu ya kuibusu asubuhi ifatayo,

Nikorome kochini matumbo yakikohoa,

Shadidi inikumbate nikauke kama aiskrimu.

Niwe Kinyago kokote,

Wa kuonwa niwe ila kusikiwa aa!

Ninyate ili guu lisiporomoshe mwendo

Nijambe ila lisinuke, niwe kimyaaa!

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top