Involvement

STR8 UP YAALIKA KIZAZI CHA GEN Z

Na Leeroy Wuone

Wanafunzi wa chuo kikuu cha Daystar shule ya mawasiliano walihudhuria hafla iliyoandaliwa Standard group mnamo Jumamosi tarehe 28 Septemba mwaka wa 2024.Wanafunzi kumi na watatu walihudhuria hafla hio iliyobandikwa jina “Siku ya ubunifu ya kizazi cha Gen-Z’’.

Lengo la Standard group la kuandaa hafla hio ilikuwa kuwahamasisha wanafunzi kuhusu mambo yanavyoendelea kwenye studio pale Standard group na ambavyo watu tofauti tofauti hushirikiana kila siku kuleta habari kemkem za hivi punde kila siku,zaidi ilikuwa siku ya kutangamana na wasanii kwenye sekta mbalimbali mfano ni anayejulikana kwa jina mluo_social.light ambaye alihudhuria hafla hiyo na kikosii chake ambao wametamba kwenye majukwaa ya mitandao ya kijamii kama Instagram na Tiktok.

Aliyetuzungusha kwenye sakafu ya kwanza “ red carpet’’ alisema kuwa uchapishaji wa magazeti ndio ulikuwa mwanzo wa the standard group kisha ikaja enzi ya televisheni na baadaye habari kwneye mitandao ya kijamii.

Kelly alipeana mfano akisema kwamba tuseme iwapo mwanahabari ametumwa kule CBK kwenye hafla ya uchapishaji wa noti mpya hawezi kuiweka taarifa hio mtandaoni bila kuwajulisha wahariri ambao wako kwenye chumba cha habari.

Kupangwa kwa red carpet ulikuwa kimkakati ndiposa waandishi wa habari hao waweze kufanya kazi kwa kijumla ili kushinda ushindani.Alitujulisha kuwa zile tahadhari za kwanza za habari hutumwa kwenye “radar desk’’ kwenye kituo cha Standard group. Lengo lao pia ni kulisambaza habari vilivyo bila kuutia chumvi .

“Checkpoint’’ ilikuwa katikati na hapo ndipo habari za kiteknolojia kama kilimo na hata mambo ya takwimu yalifanyiwa utafiti kabla habari kupeperushwa.Mfano wa takwimu ni kwa mfano idadi ya magari ambayo Wakenya hununua na magari yapi kwa idadi?

Iwapo mwanahabari ana tashwishi na utafiki wake ya nambari ataelekea kwa wanaofanya hapo checkpoint kwa usaidizi mwafaka. Alizidisha kwa kusema iwapo wanaofanya hapo checkpoint wapokee hadithi yako kama mwanahabari,wanaweza kupa takwimu zaidi ambayo ni sahihi mno.

Mwanafunzi mmoja aliuliza kuhusu watu ambao wanaendesha tarakimu zilizoandikwa kwenye runinga pale kwenye red carpet kisha alijibu ya kwamba kuna wasanidi wa wavuti ama ukipenda kwa kiingereza “web developers’’ ambao kazi yao ni kujumuisha idadi ya Wakenya wanaosoma taarifa za magazeti kwa siku moja.

Mwishowe wageni walitumbuizwa na hata kucheza densi. Watu waliweza kujifunza mengi na hata kujenga mahusiano na wakubwa katika sekta ya mawasiliano.

 

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top