Involvement

TETESI ZA SOKA ULAYA

Na Abdul Shaban

 

Nyota wa Ureno Cristiano Ronaldo

Nyota wa Ureno Cristiano Ronaldo, 37, ameafiki haja ya Manchester United ya kusaini mkataba na mshambuliaji mpya. (Express)

 

Mshambuliaji wa Manchester City Mbrazil Gabriel Jesus

Tottenham wana matumaini ya kuwapiku mahasimu wao wa kaskazini mwa London Arsenal katika mbio za kumsaka mshambuliaji wa Manchester City Mbrazili Gabriel Jesus kwa ofa ya soka ya Championi Ligi . (Mirror)

 

Raheem Sterling

Mshambuliaji wa Manchester City na England Raheem Sterling, 27, amekuwa akiwauliza watu kuhusu maisha katika magharibi mwa London huku klabu ya Chelsea ikiwa na nia naye. (Athletic)

 

Dau la awali la £21.5m kwa ajili ya Sterling limekataliwa. (Fabrizio Romano)

 

Chelsea wanaweza pia kumuhitaji mlinzi wa Manchester City mwenye umri wa miaka 27- Mholanz Nathan Ake. (Telegraph, subscription required)

 

Mshambuliaji wa Chelsea na Ubelgiji Romelu Lukaku

Mshambuliaji wa Chelsea na Ubelgiji Romelu Lukaku, 29, yuko tayari kurejea katika Inter Milan kwa gharama ya mkopo wa £8.5m pamoja na marupurupu aliyokubaliwabaina ya klabu hizo. (Mail)

 

Manchester United wanaangalia uwezekano wa kufanya dai jipya kwa ajili ya kiungo wa kati wa Barcelona na Uholanzi mwenye umri wa miaka 25 Frenkie de Jong. (Fabrizio Romano)

 

Kiungo wa kati wa Wolves na Ureno Ruben Neves

Kiungo wa kati wa Wolves na Ureno Ruben Neves, 25, yuko katika orordha ya Manchester United ya wachezaji inayoweza kusaini mkataba nao iwapo watashindwa kusaini mkataba na De Jong. (Fabrizio Romano, via givemesport)

 

Newcastle wamepewa ofa ya fursa ya kusaini mkataba na mlinzi Mivory Coast Eric Bailly, 28, kutoka Manchester United. (Mirror)

 

The Magpies pia wameambiwa kuwa ni lazima walipe £50m kusaini mkataba na winga wa Bayer Leverkusen na Ufaransa Moussa Diaby. (Sun)

 

Meneja wa Uholanzi na meneja wa zamani wa Manchester United boss Louis van Gaal alihusika kwa sehemu katika kumzuwia mlinzi wa Ajax Mholanzi Jurrien Timber, 21, kuhamia Old Trafford. (Marcel van der Kraan, Sky Sports)

 

Ajax wametenga euro milioni 40 (£34.3m) wanazotaka kuzitoza Sebastien Haller, huku Borussia Dortmund wakiwa na nia na mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27- kutoka Ivory Coast. (90min)

 

Sunderland, Huddersfield na Bristol City wameweka dau la nyongeza la have £1m kwa ajili ya kiungo wa kati Muingereza mwenye umri wa miaka 21 anayechezea klabu ya AFC Wimbledon Jack Rudoni. (Sun)

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top