Involvement

KUNA NINI KATIKA BARABARA YA MAGADI?

C21B84F3-9D5B-4371-BC87-FD7C59550353wangukanuri181152@daystar.ac.ke

Na: Wangu Kanuri

Ilikuwa vuta nikuvute katika barabara ya Magadi baina wanafunzi wa chuo kikuu cha Multimedia na polisi. Wanafunzi wa chuo kikuu hicho waliandamana na kufunga barabara hiyo kufuatia ajali iliyomlaza mmoja wao katika hospitali kuu ya Kenyatta huku akiwa katika hali mahututi. Kamanda wa Langata bwana Gregory Mutiso aliwarai wasafiri kutumia njia mbadala wanapowatuliza wanafunzi hao waliokuwa wamekabwa koo. Ajali katika barabara hiyo zinazotamatisha maisha ya wanafunzi katika chuo kikuu hicho si jambo geni ndio maana maandamano hayo yaliyoonyesha kughadhabishwa kwa wanafunzi na madereva.

Kwa kutaka kuchukulia haki mikononi mwao kwa mwanafunzi huyo aliye katika mwaka wake wa kwanza na ambaye wiki jana aligongwa na yu katika hali mahututi, wanafunzi hao waliokerwa walistahimili vitoa machozi ambavyo maaskari waliwarushia nao wakiwarushia mawe. Mwanafunzi huyo aligongwa na matatu iliyokuwa ikiendeshwa kwa kasi mno hapo karibu na lango la chuo hicho kikuu. Isitoshe wanafunzi hao walilalamikia polisi kwa kuchelewa kushughulika baada ya mwanafunzi huyo kugongwa.

Uchungu uliokuwa nyoyoni mwa wanafunzi hao ulidhibitisha kuwa walikuwa wamekerwa na ajali zinazofanyika katika barabara hiyo zinazotamatisha nyoyo za wenzao huku wakikumbuka kuwa mwaka wa 2016 walipoteza wanafunzi  wawili katika barabara iyo hiyo. Zaidi ya hayo, walilalamikia kuongezewa kwa nauli kwa matatu ya tume ya Ongataline na kunyanyaswa na waendeshaji wa magari hayo.

Japo gari hiyo iliyomgonga mwanafunzi hiyo I katika kituo cha polisi, usakaji wa dereva huyo aliyemgonga mwanafunzi huyo bado waendelea. Hali kadhalika wanafunzi watatu walikamatwa katika maandamano hayo.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top