Involvement

Tetesi Za Mbappe

{Picha kwa hisani ya Sky News}

 

Na Abdul Shaban

 

Mshambuliaji Kylian Mbappe wiki jana Jumanne aliripotiwa kuwa na kikao maalumu na rais wa Paris Saint-Ger-main, Nasser Al-Khelaifi kujadili hatima yake.  Rais wa PSG Al-Khelaifi alikiri kushtushwa na uamuzi wa mshambuliaji huyo kwamba hawezi kubaki kwenye timu hiyo hadi 2025. Kutokana na hilo, PSG ilimpa Mbappe wiki mbili za kuamua kama anabaki Parc des Princes kwa maana ya kusaini mkataba mpya au la basi auzwe kwenye dirisha hili hili la uhamisho wa majira ya kiangazi.

Hivyo, Mbappe na Al-Khelaifi walitarajia kukutana jana ana kwa ana ana kwa ajili ya mazungumzo na kuwekana wazi juu ya hatima ya kila upande klabuni hapo. . Kuna ripoti zilidai kwamba Mbappe atakwenda kuambiwa hadi kufikia Julai 31 atatakiwa aweke wazi msimamo wake kama atabaki PSG hadi 2025 au milango ifunguliwe ya kupokea ofa ya kupiga bei mwaka huu.

Real Madrid bado wanapewa nafasi kubwa ya kunasa saini yake, lakini miamba hiyo ya Bernabeu inaelezwa kwamba haina pesa za kugharimia uhamisho wake baada ya kumtumia mkwanja mrefu kwenye dirisha hili kunasa huduma ya kiungo Jude Bellingham kutoka Borussia Dortmund. . Kutokana na hilo, timu za Ligi Kuu England zinaweza kuingia kwenye mchakato wa kunasa saini yake ikiwamo Manchester United, Arsenal na Liverpool ambazo zote zimeripotiwa kufuatilia kwa karibu mchakato huo.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top