Involvement

Ligi kuu ya mabingwa barani Ulaya

(Picha kwa hisani ya SoccerBible)

 

Na Dennis Mungai

Raundi ya pili za mechi za makundi ligi ya mabingwa barani Ulaya itaendelea wiki hii. Siku ya Jumanne mechi nane zitachezwa, ya kwanza ikiwa kati ya Union Berlin na Braga ya Ureno. Vijana wa Erik ten Hag Manchester United wataialika Galatasaray huku wakitafuta ushindi wao wa kwanza katika kundi lao.

Mabingwa watetezi wa ligi ya Italia Napoli watakua wenyeji wa Real Madrid nayo Arsenal itasafiri hadi Ufaransa kumenyana na Lens.  Copenhagen watachuana na Bayern Munich, Inter dhidi ya Benfica nayo PSV watacheza na Sevilla. RB Salzburg watakua wataialika Real Sociedad ya Uhispania.

Siku ya Jumatano Borussia Dortmund watachuana na AC Milan huku Celtic wakipambana na Lazio. Baada ya miaka ishirini nje ya michuano hizi, Newcastle United wana kibarua kigumu dhidi ya Paris St Germain ugani St.James Park. Baada ya kushindwa na Wolves siku ya Jumamosi, Pep Guardiola anatarajia ushindi kutoka kwa Man City watakapocheza na RB Leipzig ya Ujerumani.

Atletico Madrid wataialika Feynoord nayo Porto watakua wenyeji wa vijana wa Xavi Hernandez ,Barcelona.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top